Posts

Showing posts from October, 2022

SHAMBA LA CHUMVI LANAWIRI TENA

Ilikuwa ni Muda ambao Ndoto ya mpwani kuimarika ilititiliwa kikomo kusawazisha mahangaiko,maisha duni,Uhuni na hali zisizoeleweka Kwa ujumla. Bandari ya mombasa ni moja ya kitega uchumi eneo bunge hilo na hata taifa zima la kenya na hii imekuwa faida kuu kwa wakaazi eneo bunge hilo ambao wamenawiri kupata ajira na kupanua biashara zao kwa kipindi cha miaka mingi. Kwenye serikali iliyotoka mamlakani mambo hayakuwa sawa kwa mpwani kwa amri iliyotolewa ya uhamisho wa almashauri ya bandari kutoka mombasa Hadi naivasha Kwa misingi isiyopo na Majibu .Kulingana na Wengi waliitamka kama dhulma ya kuwafaidi matajiri na kuwaponza maskini .Hili lilizua mchepuko mkubwa  Kwa wakaazi kwani walihisi kutolewa Tonge mdomoni. Waajiriwa wengi wakakosa nafasi za kazi kwa kuwepo sheria ya usafiri wa shehena ya mizigo kupitia reli kinyume na vile Ilikuwa kama zamani pale lorry la trela lilitumika kufanya shuhuli hii.maderava Wengi Unga Wao ukamwagika . Kampuni nyingi Ambazo ziliitegemea bandari hii kwen...

MAPENZI SHIKAMOO VYUONI

Image
Kwenye kumuumba Binadamu Mwenyezi alimpa upendo kama njia moja ya kuchepua mahusiano na kuwaleta karibu viumbe wake. Kwenye zama za wazee wetu mapenzi yalidhihirishwa kwa njia kuu sana na kubebwa ghali kama hata ilivyoandikwa kwenye bukrata takatifu.wazee wetu wangeweza kuwapenda wapenzi wao penzi la dhati au tuseme lile penzi tunaloliskia la romeo and Juliet. Enzi hizi za karne ya ishirini na mbili inashangaza sana mapenzi yakiwa  kama silaha ya chuki, kuumizana na hata kutoana roho kwasababu zisizoeleweka . Tukizamia Kwa umri Wa mabarobaro vijana haswa walioko kwenye vyuo vikuu wamejipata kwenye tabu ya bahari hii ya mateso iitwayo mapenzi.Sijui mimi Akili nyingi labda sifahamu mapenzi ni nini lakini jinsi wengi wanavyobakia hoi inashangaza sana. Vijana wanaanza kwa kuwa na mazoea kama njia moja ya kufahamiana tu alafu kwa kipindi kifupi kunazuka uhusiano mkubwa Wa mtu kutopata Usingizi asipimuona au kuzungumza na Mwenzake nafkiri tunajua fika mazoea yana tabu. Ghafla...

FIKRA ZA KICHAWI

 Tunajivunia Nchi Yenye Mandhari,Raslimali na Wananchi Wenye Bidii Na Maona Ya Juu Kwa Sana Lakini vyote Hivi vinageuka Kuwa Maini Chungu ,Hasira ,Fujo na ubaguzi Wa Kikabila Pamoja na tabaka Kwa Sababu ya Hawa vigogo wasimamizi tunaowaita "Viongozi " Uongozi hasa kwenye Uwanja Wa Siasa ni Jambo la utata ambalo hujaa Uongo, Chuki na Hata kumwaga Damu Kwa Kiwango Cha Ajabu Labda Niseme Hata kutoana Kafara. Wanasiasa Wengi Nchini wametamalaki kwenye Akili zetu na Hata kumiliki nyoyo Zetu Kuifanya Damu kuchemka Kila tunapomsikia raia mwenzetu akimzungumzia Kiongozi aliye wako. Ikumbukwe nchii hii mnamo Mwaka Elfu Mbili na Saba Damu ilitapakaa Kila mahali ,Mali kuaribiwa na Hata makabila kuchukiana Swala Hatari Zaidi lilisobabisha maelfu ya Watu Swala Kuu likuwa Hawa Viongozi Wetu. Jamani kwani kumpenda Kiongozi Wako Kuna msukumo upi unaolenga Mpaka kumchukia Jirani Yako Mnagombana Chumvi Kila Siku...? Hapo Mimi Akili nyingi Nakosa Jibu . Kilichofichika Nikuwa Hawa Wanasiasa Mcha...