Posts

Showing posts from May, 2023

VUGU VUGU MOMBASA YAONGOZA MAANDAMO.

Image
.      ( Picha ya waandamanaji ) Kundi la vugu vugu Mombasa pamoja na wananchi, wameongoza maandamano ya Ili kuwasilisha matakwa wanayoyasema kuwa ya utetezi wa haki kwa wananchi Mombasa kwake gavana    Abdulswamad Shariff Nassir .      Picha ya Michael Nato akihojiwa  Kwenye mahojiano na wanahabari,msemaji wao mkuu bwana Michael Nato, ameiponda serikali ya kaunti kwa kuingilia mipango ya wafadhili wanaowasaidia wananchi haswa kwenye maswala ya afya . .     ( Picha ya hoja zilizowasilishwa Kwa              gavana ) Akizidi kuzungumza, ameyataja maandamano Hayo Kuwa ya kilio Cha wananchi wa mombasa ambao wanaozidi kuumia wakati wafadhili wanapigwa vita haswa kipindi cha wakati mgumu. .      ( Picha ya hoja zilizowasilishwa kwa              gavana ) Kwenye kuwasilisha hoja, Nato amezungungumzia haki za wafadhili na kutaka she...

POLISI WANASA BANGI CHANGAMWE

Image
 (Picha ya misokoto ya bangi ikiwasilishwa kituo Cha Polisi) Mlanguzi sugu wa dawa za kulevya kwa Jina maarufu ( Mama Irene ) amefumaniwa na maafisa wa polisi katika kaunti ndogo ya changamwe eneo la dunga unuse kisha kutoweka kupitia mlango wa nyuma wa duka lake baada ya kupatikana na misokoto kadhaa ya bangi ambayo dhamana yake ni takriban shilingi elfu sitini. . (Picha ya misokoto ya bangi) Hili limetokea baada ya uchunguzi mkali uliotekelezwa na maafisa wa polisi walioshiriakiana na raia Ili kufikia eneo lake la biashara .  (Picha ya misokoto ya bangi kwenye duka la mlanguzi) Mkuu wa oparesheni hiyo, ambaye ni ACC wa changamwe bwana Nicholas Kaito ameeleza jinsi mlanguzi huyo alivyoponea tundu la sindano baada ya kutoweka ila msako mkali wa kumtafuta unaendelea.   ( Bwana ACC Akiwa na Mmoja Wa wanunuzi) Pia , ametangaza onyo kali kwa walanguzi wa mihadarati wanao jificha mitaani pamoja na kuwaomba wananch...

VUGU VUGU MOMBASA YATISHIA SERIKALI YA KAUNTI KWA KUZUILIA UFADHILI.

Image
Kundi la vugu vugu Mombasa limeandaa Mkutano Wa wanahabari Katika Hospitali kuu ya makadara Siku ya Leo lengo lao kuu likiwa kuangazia swala linalohadhiri jamii kwa sababu ya hatua ya serikali ya kaunti ya mombasa kuzuia ufadhili Wa mombasa cement kuwasaidia wananchi haswa wanapolemewa na madeni kwenye hospitali hiyo. Msemaji mkuu  Bwana Michael Nato Amemkashifu vikali Gavana wa kaunti hiyo  Abdulswamad Nassir  kwa kusema kuwa ni unyama kupinga hatua ya msaada uliokuwa ukiwashika mkono sana wakaazi wengi wenye kipato cha chini haswa kwenye maswala ya Malipo hospitalini humo  . Akiuliza ,Nato ametaka kujuwa ni sera ipi kaunti imetumia Ili kuhafikia kuzuia ufadhili na pia ni nia Gani wanayopania Kwa mwananchi...? Mmoja Wa wahadhiriwa amesimulia jinsi alivyokatishwa tamaa Wakati alifiwa na Mamake mzazi na Wakati anatafuta msaada Wa Malipo ya hospitali Akapata Barua ya usimamizi Wa mfadhili Mombasa cement Jambo lililomfanya kuhangaik...