MASTAR WA DESTINY WASHINDA KWENYE CHANGAMWE TALENT SEARCH
Changamwe Talent Search ilitangulizwa na mchujo kwenye wadi tofauti ikiwemo: Changamwe,Chaani ,Kipevu, Airport na Portritze ambapo washindi wawili Kila wadi waliteuliwa kwenye fainali kumenyana na wenzao bomu stadium.
Mazoezi yamekuwa ya uangalifu mno pale waandalizi wakuu walishirikiana na vitengo tofauti Vya Sanaa :Kusakata ,kuigiza ,Shairi ,na Kuimba Ili kuhakikisha Kila mwaniaji Yupo kwenye Njia sawa na atazifwata sheria zinazostahili
Vijana Wa destiny international home of Talents Muda Huu Wamekuwa wakitia Bidii kwenye mazoezi huku wakijuwa mtaka Cha mvunguni sharti ainame.Wamekuwa wakinoa Makali kwenye Kusakata densi ,uigizaji na Shairi vitengo ambavyo Wamekuwa na umakinifu navyo.
Kwenye fainali ni maajabu yamefanywa hapa ndipo wale wasanii ibuka wamechana mistari kuwaacha mashabiki Kwa shangwe na mshangao. Vijana Wa destiny walifunika Zaidi Kwa vitengo vyao na kujizolea vikombe vitatu ,vyeti vitatu na elfu Kumi na tisa Pesa taslimu .kundi ambalo lilizoa zawadi nyingi na Kuwa mshindi Mkuu Kwa jumla.
#Akilinyingi.
#fikrazakichawi.
#Mombasa.
Comments
Post a Comment