MAQDIS FC NDIO MABINGWA RABAI TALENT CUP


.   Picha ya wachezaji wakimenyana. (Maqdis ni Wenye jezi nyeupe na kaptura nyeusi na power ni yenye jezi nyekundu na kaptura ya kijani.)

Maqdis fc wameibuka mabingwa wa fainali  ya Rabai Talent cup, baada ya kuinyuka timu  ya Power United mabao 3-2 katika uwanja wa Mgalla wadi ya rabai kisurutuni Katika eneo bunge la Rabai Kaunti ya Kilifi.
  ( Picha ya Kamoti Junior Mwenye shati nyeupe akikagua wachezaji)
Michuano hiyo Iliandaliwa na Kamoti Saburi maarufu  Kamoti Junior kwa ajili ya kuwaleta vijana pamoja na kuinua vipaji vyao vya soka, timu 32 zilishiriki michuano hiyo.   
(picha mchezaji Wa power akichapa mkwaju wa ikabu)
Kwenye fainali hiyo vijana wa timu ya   Maqdis walionyesha ujasiri baada ya kutoka nyuma na kuchukua ubingwa dhidi ya miamba Power United waliotangulia kuliona lango dakika za mwanzo wa kipindi cha kwanza. 
Timu ya Maqdis imeweza kutwaa taji hilo kupitia mkwaju wa penalti na kufanya matokeo kuwa 3-2.

.   ( Picha Kamoti Junior akizungumza )
Kamoti ameweza kuwapongeza vijana hao kwa kuonyesha nidhamu na bidii kwenye tasnia hiyo ya soka na kufanya mashabiki kuhemka kwa furaha. 

Timu zote zimeweza kupata zawadi mbali mbali ikiwemo vikombe, jezi ,mipira na pesa taslim elfu 20,000.

Aidha fainali hiyo ilichachishwa zaidi baada ya mbunge wa eneo hilo Anthony Kenga Mupe kuwasili na kuweza kuzidi kuwapa motisha wachezaji na vijana kwa jumla.
(Picha mbunge Kenga Mupe akizungumza )
Mbunge huyo, ameipa talanta kipaumbele na kuahidi kuanzisha michuano itakayo shirikisha timu eneo bunge lote la Rabai Kenga Wehu Super cup itakayo zinduliwa mwishoni mwa jumalijalo.

Kenga aidha amewasihi vijana kutojihusisha na  dawa za kulevya na badala yake wajihusishe na michezo akisema kwamba dawa hizo zina athiri nyota zao za maisha ya usoni.

Wakati huo huo ,Kenga amewasihi walimu kutowatuma wanafunzi  nyumbani  kwa sababu ya ukosefu wa karo akisema kuwa afisi yake inaweka mikakati ya ufadhili wa elimu ili wanafunzi wapate kusoma bila tashwishi.

Mbunge huyo , ametaja kuwa uhaba wa maji unaoshuhudiwa katika eneobunge hilo na akahakikisha kuwa serikali ya kaunti pamoja na serikali kuu wapo  kwenye mchakato  ili swala hilo kutatuliwa ipasavyo.

"nitahakikisha serikali ya kitaifa na ile ya kaunti zinalishugulikia kwa haraka tatizo hilo ambalo limekuwa miaka nenda miaka rudi", alisema.
Mwisho.



© AKILINYINGI
    MOMBASA 

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

VIJANA KAZINI

POLISI WANASA BANGI CHANGAMWE

EPZ CHANGAMWE YAFUTA WAFANYIKAZI GHAFLA.